Thursday, January 08, 2015

PROFESA TIBAIJUKA AWAMBIA WANANCHI KUTENGA SIASA NA MASUALA YA MAENDELEO



NA AUDAX MUTIGANZI
MULEBA

Mbunge wa jimbo la MULEBA kusini PROFESA ANNA  TIBAIJUKA ameshauriwa wananchi katika jimbo hilo kuwapuuza wanaochanganya masuala ya siasa na masuala ya maendeleo  hasa wale wanaobeza mambo yanayobuniwa na viongozi  yenye lengo la kuboresha maisha hali zao za maisha.

PROFESA TIBAIJUKA ametoa ushauri huo wakati semina ya siku MOJA iliyofanyika kwenye ukumbi wa jengo la taasisi ya KAJUMULO  ulioko wilayani  MULEBA ambayo iliandaliwa na mbunge huyo kwa  wafanyabiashara na wakulima wa zao la ndizi katika jimbo la hilo ambayo  ilikuwa na lengo la kujadili mikakati ya kuhakikisha zao hilo linakuwa na soko la uhakika.

Mbunge huyo ambaye alikuwa waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi amesema masuala  ya maendeleo  hayaendani na  itikadi za  kisiasa, amewakemea wanaodhani kwamba kwa sasa amejikita katika   masuala ya kuwaletea maendeleo wananchi kwa lengo la kujiongezea umaarufu.

INSERT No.1……Profesa Anna Tibaijuka……Mbunge wa Muleba kusini

ELIUD  ISHABAKAKI, GIBSON MUGANYIZI, SIMON  MBALULA na  STEVEN ANGELICUS  ni miongoni mwa wafanyabiashara na wakulima wa ndizi walioudhuria semina hiyo wanaoeleza  hali ya soko la ndizi, changamoto wanazokabiliana nazo na pia wanatoa ushauri kwa serikali, huku  EDMUND KATANGAYO akiwahimiza wananchi katika jimbo kubuni fursa mbalimbali zinazoweza kuwaondoa katika wimbi la umaskini.

No comments:

Post a Comment