Tuesday, December 30, 2014

Mpasuko ndani ya Yanga.Manji aingia mgogoro mwingine na secretariat




-Awafunga watumishi Yanga: Aagiza Polisi ‘Marafiki’ kuwakomesha
Baada ya kumtimua kocha Mkuu wa timu yake na baada ya kubwaga chini sekretariati ya klabu hiyo, Mwenyekiti wa Klabu ya Young Africans Sports Club (Yanga) Bw. Yusuf manji, ameamua kuwafanyizia baadhi ya waliokuwa watumishi wa Klabu hiyo akiwemo Beno Njovu, Katibu Mkuu aliyepita.
Wakandamize haswa
Kulingana na mawasiliano yaliyonaswa na makachero wetu kati ya Mwenyekiti huyo na viongozi wa juu wa Klabu hiyo, Manji amewapa maelekezo wanasheria wake na Sekretariati ya sasa kuwafungulia mashtaka Sekretariati iliyopita  kwa madai  ya  ufujaji pesa, huku akiwataka viongozi hao kutumia ‘marafiki’ zao waliooko katika jeshi la polisi ‘kuhakikisha wanashugulikiwa’

Katika mawasiliano hao kupitia email ya tarehe 22 Desemba , Manji pia anamwagiza mtu aliyetambulika kuwa mhasibu  anayaenda kwa jina la Amit kugaramia ‘maagizo hayo yote’, na kumpa taarifa kila siku.
Vyombo vya habari kutumika
Manji pia  ameagiza wafanyakazi hao wazamani ‘wachafuliwe’  kupitia kampeni kali magazetini, huku akielekeza ‘Press Release’ yenye saini yake itolewe ikionesha ‘masikitiko yake’.

Adhabu mbele, hukumu nyuma
Huku akitoa maagizo wafanyakazi hao washugulikiwe ipasavyo na polisi ‘marafiki’ zake, Bwana Manji ametupilia mbali haki za wafanyakazi hao kusikilizwa kukiwa hakuna uchunguzi wowote uliokwishafanyika kuhusu madai yake dhidi ya watumishi hao zaidi ya hisia zake mwenyewe na Sekretariati mpya inayotekeleza kila alitakalo bila kuhoji.

 Maagizo yazua mpasuko ndani ya kamati tendaji
Kufuatia maagizo ya Manji, mmoja wa watumishi wapya aliyetambulika kama Frank Chacha alitekeleza maamuzi hayo ambayo mwenyekiti huyo alikuwa amesema hayapingiki wala hayahojiki kwa email yake, huku wakifungua kesi katika kituo cha Polisi kati Dar es salaam na kufanikiwa kuweka wafanyakazi wawili ndani huku wakiendelea kumuwinda Beno Njovu
Lakini masaa machache baada ya hatua hizo, kuna dalili kuwa baadhi ya viongozi ndani ya klabu hiyo wanapinga vikali hatua hizo za Manji na wametishia ‘kuaachia’ ngazi.
Mpasuko huo ndani ya Yanga umedhihirishwa na email kutoka kwa Bwana Omar, Mkurugenzi mpya wa Fedha na Utawala akimjulisha Manji kuwa jana Jumanne, baada ya kutekeleza maagizo ya Mwenyekiti huyo alipokea simu kutoka kwa  Isaac Chanji, mjumbe wa Kamati Tendaji akitishia kuwa  hatua ambazo zilikuwa zimeshachukuliwa zilikuwa za hatari kwa Klabu hiyo na kuwa yeye Chanji na wajumbe wengine wengelazimika kuwaachia akina Omari na Chacha timu hiyo.

Maswali tata
Kufuatia hatua hii ya Manji mtu unaweza kujiuliza maswali kadhaa:
1.       Je kwa nini Yanga inakuwa na kesi kila wakati? Gharama za kesi hizi, ambazo nyingine siyo za lazima, si mzigo usiokuwa na faida kwa Yanga? Mara wachezaji, makocha, na Sekretariati za nyuma.
2.       Ni dhahiri kuwa hata kama kesi hii ya sasa ina msingi wowote, basi uchunguzi ungetangulia. Lakini, labda kwa jeuri ya hela, Manji ameshawahukumu watumishi wale na ni wazi kuwa yuko tayari hata kupindisha sheria ili afikie lengo lake.
3.       Lengo la Manji hasa ni nini? Anajaribu kuwaadhibisha hawa watumishi kweli au ni kujenga hoja za Mkutano Mkuu wa Klabu hiyo unaotegemewa kufanyika Januari 2015 kwa kujenga mazingira ya kuwasahaulisha wanachama wa Yanga baadhi ya  ahadi alizotoa na ambazo hadi sasa bado ni ahadi hewa  tu?


No comments:

Post a Comment