Saturday, February 15, 2014

UONGOZI WA FREEMEDIA MATATANI

Uongozi wa gazeti la Tanzania daima umepewa majuma mawili kuwaomba radhi wananchi wa vijiji vya Kiga na Buhanga vilivyoko wilayani Muleba kwa kukanusha taarifa lilizozichapishwa na gazeti hilo  juma lililopita wanazodai kuwa zililenga  kuwadhalilisha, kuwachonganisha  na kuwagawa  wananchi na viongozi wao.
 
Viongozi waliotoa kauli hiyo ni pamoja na Masoud Ibrahim ambaye ni mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Kiga na Dominic Domician mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Buhanga kwa niaba ya wananchi ambao walisema ikiwa uongozi wa gazeti hilo hautawaomba radhi  wananchi wa vijiji hivyo  katika kipindi hicho watafikia uamzi wa kulifikisha mahakamani.
 
Wakiongea na gazeti hili jana walisema gazeti hilo liliwadhalilisha wananchi kwa kuchapisha taarifa iliyokuwa inadai kuwa wananchi wa vijiji hivyo walioungwa pilau na waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka alipofanya mikutano ya hadhara kwa nyakati tofauti katika vijiji hivyo hivi karibuni.
 
Walisema taarifa hiyo iliyochapishwa kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti la Tanzania Daima kuwa ilikuwa sio ya ukweli bali ilikuwa  ni ya uzushi kwa kuwa pilau iliyoliwa na wananchi  wakati Profesa Tibaijuka ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Muleba Kusini alipotembelea vijiji hivyo ilikuwa imeandaliwa na wananchi wenyewe kuwa wala yeye hakuusika.
 
“Profesa Tibaijuka alipofika kwenye kijiji changu cha  Buhanga alikuja kuhamasisha maendeleo na mgeni yoyote akikutembelea ni lazima mkaribishe sisi wahaya tunasema ‘akamwani’ mimi nashangaa makaribisho tuliyomfanyia waziri watu kuyatafsiri vingine, hakuandaa pilau bali pilau tuliiandaa sisi viongozi na wananchi” alisema Dominic kwa masikitiko.
 
 
“Nini ninachoshukuru alipofika katika kijii Buhanga aliazimia kujenga vyumba vinne vya madarasa katika  shule ya msingi ya Rulanda, shule ilikuwa katika hali mbaya wanafunzi walikuwa wakitumia vyumba vya madarasa vilivyojengwa kwa udongo na kuezekwa kwa nyasi, ninachosema ziara yake katika kijiji change ilikuwa na mafanikio nashangaa wanaombeza” alisema Dominic.
 
 
Masouud Ibrahim, mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Kiga alisema kunapowachafua viongozi tuwakatisha tama hata mambo mazuri wanayokuwa wameyapanga kuwafanyia wananchi wanalazimika kuyasitisha, aliviomba vyombo mbalimbali vya habari viandike mambo mazuri wanayoyafanya  viongozi badala ya kuandika habari zinazolenga kuwakatisha tama viongozi hasa wanaofanya harakati kubwa za kuwaletea wananchi maendeleo.
 
Alisema kuwa Profesa Tibaijuka ni mhamasishaji namba moja wa masuala ya maendeleo, aliendelea kusema wanaomsema vibaya wanalenga kumkatisha tama, aliwaomba wananchi katika jimbo la Muleba Kusini kupuuza propaganda mbalimbali zinazolenga kumchafua Profesa TIbaijuka.
 
 
Masoud aliwaomba wananchi kumuunga mkono kila jambo linalobuniwa na Profesa TIbaijuka lenye lengo la kuwaletea maendeleo, alisema kuwa watu ambao kawaida yao ni kupinga kila lililozuri ambao linaweza kuleta ustawi ndani ya jamii.
 
Viongozi hao waliwaomba pia wananchi katika vijiji hivyo kuwa na mshikamano ili waweze kudumisha amani na upendo ndani ya jamii.
 

No comments:

Post a Comment