Thursday, February 20, 2014

MKOA WA KAGERA WAPEWA SOMO JUU YA KUPUNGUZA TATIZO LA AJIRA NA KUKUZA UCHUMIWA MKOA




Kupitia serikali ya Ujerumani mkoa wa Kagera umepata mtaalam mshauri ambaye anatoa utaalam wa kuusaidia mkoa katika nyanja mbalimbali za kuinua uchumi wake kwa kutoa ushauri jinsi ya kutumia fursa zilizopo mkoani Kagera kwa ajili ya kuleta maendeleo ya haraka kwenye jamii.
Bw. Joern Bernhadt   ni mtaalam aliyebobea katika kutoa ushauri wa  huduma za jamii kwa miaka 41 kutoka nchini Ujerumani na amewahi kufanya kazi katika nchi mablimbali kama Indonesia, Swaziland, na Ethiopia.
Bw. Bernhadt alikutana na Mkuu wa Mkao wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe pamoja na Wataalam kutoka katika ofisi yake na kutoa ushauri wake juu ya kongeza ajira katika mkoa wa kagera pamoja na kuendeleza watu wa ngazi ya chini kielimu kupitia vyuo vya ufundi.
Katika kutengeneza ajira Bw. Bernhadt alipendekeza Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwa zinaweza kuamua kujenga barabara za mawe ambazo kwa kiwango kikubwa zinatengeneza ajira kwa watu wengi na kudumu kwa muda mrefu alitolea mfano wan chi ya Ethiopia ilivyopunguza tatizo la ajira kwa njia hiyo.
“Katika kutengeneza barabara hizo wananchi watafundishwa jinsi ya kuchonga mawe na baada ya mawe hayo kuchongwa yatanunuliwa na serikali ili itengeneze barabara na kwa kufanya hivyo tayari wananchi ambao hawana ajira wanaweza kujiajili kupitia miradi kama hiyo”. Alishauri Bw. Bernhadt.
Elimu, Mtaalam huyo aliashauri vyuo vya ufundi kujengwa vingi iwezekanavyo ili wananchi wengi wapate ujuzi wa ufundi. Lakini alitaadharisha kuwa katika vyuo hivyo soko ndilo litaje ni huduma gani inahitajika ili walimu watoe elimu sahihi ya kukidhi soko husika na siyo kufundisha ufundi tu.
Uchumi, katika kukuza uchumi  wa mkoa Bw. Bernhadt alipendekeza serikali kuweka njia rahisi za kuwafanya wananchi walio wengi kuanza kufanya biashara kama kuweka njia fupi za kupata leseni na kupata bidhaa kwa urahisi zaidi ili kushawishi mazingira rafiki kwa biashara.
Aidha kushawishi nchi jirani kama Rwanda, Burundi na Uganda kuwekeza katika masuala ya usafirishaji kama kuanzisha safari za ndege kutokea Bukoba kwenda Entebe, Kigali na Bujumbura kwasababu mkoa wa Kagera ni kitovu cha nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Bw. Bernhadt alimalizia kwa kuwakumbusha wataalam wa mkoa wa Kagera kuwa ili kutoa huduma nzuri kwa Jamii siyo lazima uwe na mtaji mkubwa sana wa fedha mfano huduma ya afya, alishauri kwa wananchi wenye tatizo la kutembea muda mrefu kutafuta huduma  wanaweza kujengewa vituo vidogo vya kupatiwa huduma ya kwanza kabla ya kufika katika vituo vikubwa  vya kutolea huduma za afya.
Imeandaliwa na:
Sylvester Raphael
AFISA HABARI
RS-KAGERA@2014


No comments:

Post a Comment