Saturday, November 30, 2013

Ndege iliyopotea Msumbiji yapatikana


 
Ndege hiyo ilitakiwa kutua kwenye uwanja wa Luanda.
Ndege iliyopotea tangu jana baada ya kuruka kwenye anga ya Msumbuji kuelekea Angola ikiwa na watu 34 imepatikana katika mbuga za wanyama Kaskazini Magharibi mwa Namibia.
Msemaji wa Polisi nchini Namibia amesema ndege hiyo iliteketea yote huku kukiwa hakuna aliyenusurika.
Ndege hiyo namba TM470 iliondoka Maputo nchini msumbiji tangu siku ya ijumaa na ilikuwa ikielekea Luanda nchini Angola.
mabaki ya ndege hiyo iliyoteketea kabisa yamepatika kwenye mbuga ya wanyama Bwabwata karibu na mpaka wa Angola na Botswana.
"Ndege imeteketea yote yamebaki majivu tu hakuna hata mtu mmoja aliyenusurika," Naibu Kamishna wa Polisi nchini Namibia Willy Bampton amenukuliwa na shirika la habari la Reuters.
Inaelezwa kuwa masiliano ya mwisho na ndege hiyo yalikuwa ni wakati ndege hiiyo ilipofika kaskazini mwa Namibia.
Kwa mujibu wa shirika la ndege la Msumbiji abiria walipanda ndege hiyo ni raia 10 wa Msumbiji, Angola 9, Wareno 5, Mfaransa 1 , Mbrazili 1 na Mchina 1.
Jopo la watu waliokuwa akifanya kazi ya kuitafuta ndege hiyo walishindwa kuingia kwenye mbuga hiyo hapo jana baada ya mvua kubwa kunyesha kufanya barabara kushindwa kupitika.
Abiria 28 na wafanyakazi sita walikuwa kwenye ndege hiyo wakitoka Maputo kuelekea Luanda.

No comments:

Post a Comment