Tuesday, November 12, 2013

MJUMBE WA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA AFARIKI DUNIA NCHINI AFRIKA YA KUSINI


Marehemu Dkt. Sengondo Mvungi aliyekuwa Mjumbe wa Mabadiliko ya Katiba nchini Tanzania
Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini Tanzania imepata pigo baada ya mmoja wa wajumbe wake Dr. Sengondo Mvungi kufariki dunia nchini Afrika Kusini, ambako alikuwa akitibiwa.
Dr. Mvungi, alipelekwa Afrika Kusini kwa matibabu zaidi baada ya kuvamiwa na watu wanaoaminika kuwa majambazi nyumbani kwake mjini Dar, es Salaam, wiki iliyopita.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Assaa Rashid Dkt. Mvungi alifariki majira ya saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini akiwa katika Hospitali ya Milpark.
"Kwa masikitiko makubwa, Tume inawafahamisha wananchi kuwa Mjumbe wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyekuwa akipata matibabu katika Hospital ya Milpark iliyopo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini amefariki dunia leo Jumanne, Novemba 12, 2013 saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini," amesema Bwana Rashid katika taarifa yake fupi.

No comments:

Post a Comment