Wednesday, October 30, 2013

RAIS KIKWETE ASHAURIWA MAMBO YA KUNUFAISHA NCHI


Kufuatia hatua ya marais wa baadhi ya nchi zinazounda jumuia ya Afrika Masharik, Kaguta Mseveni, Paul Kagame na Uhuru Kenyatta ya kufikia makubaliano ya matumizi ya vitabulisho vya uraia kutumika badala ya Passport na masuala ya usafirishaji wa mizigo kwa njia ya bandari  baadhi wananchi  mkoani Kagera wametoa maoni yao juu ya uamzi huo.

Wakiongea kwa nyakati tofauti wamesema uamzi wa viongozi hao unaashiria kuvunjika kwa mara ya pili kwa jumuia ya afrika mashariki , jumuia ya kwanza iliyokuwa imeimarika kiuchumi ilivunjika mwaka 1977, ambayo  ilifuatia mismamo tofauti ya marais wa nchi waliokuwa wananchama ambao ni pamoja na hayati mwalimu, julias Nyerere, Idd Amin na Jomo Kenyatta.

Wananchi hao wanasema kiama cha jumuia ya sasa kinakaribia kwa kuwa kuna masuala ambayo Tanzania kamwe haitakubali yaingie kwenye masuala ya kiitifaki ya jumuia hiyo ambayo nia pamoja na suala la ardhi.

Wanaendelea kusema kuwa nchi nyingi zilitegemea ardhi inayomilikiwa na nchi za jumuia hiyo kuwa itakuwa  mali ya nchi wanachama, hali hiyo ingewawezesha wananchi wa jumuia hiyo toka nchi moja kwenda nyingine kutafuta ardhi.

Tanzania ni moja ya nchi yenye ardhi kubwa miongoni mwa nchi hizo, hivyo kila nchi inatafuta namna ya kunufaika na ardhi ya nchi yetu, uamzi wa viongozi wa nchi Tanzania wa kutokubali kuiachia ardhi ndio unawaudhi baadhi  viongozi wa nchi wanachama.

Nchi nyingi za jumuia hiyo zina ardhi ndogo ambayo hazikidhi matakwa ya wananchi wa nchi hizo kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji, walitoa ushauri kwa Rais Jakaya Kikwete akiganganie nchi yetu iwe  mmoja wan chi za jumuia ya afrika mashariki, walishauri aiondoe nchi yetu.

Walisema baadhi ya viongozi wa nchi  jumua ya afrika mashariki walilenga zaidi kukopa rasilimali zinazopatikana katika nchi hii, propoganda zote hizo ni baada ya kuona  mipango yao kukopa rasilimali zilizoko katika nchi imekwama,  ndio sasa zinatafuta namna ya kuitenga Tanzania kama namna ya kuitisha itekeleze matakwa ya viongozi wa nchi hizo.

No comments:

Post a Comment