Sunday, October 27, 2013

Jeshi la DRC lakomboa miji mitatu


Mpiganaji wa M23 Rutshuru
Jeshi la Jamhuri ya Demokrasi ya Congo linasema limeikomboa miji miwili mengine kutoka kwa wapiganaji wa M23, karibu na mpaka wa Rwanda.
Jeshi liliwaambia waandishi wa habari kwamba Jumapili limeteka Rutshuru na Kiwanja, katika jimbo la Kivu kaskazini; baada ya kuteka Kibumba Jumamosi.
Umoja wa Mataifa unasema mwanajeshi mmoja wa Tanzania, katika kikosi cha kuweka amani cha Umoja wa Mataifa, aliuwawa Kiwanja, akijaribu kuwalinda raia.
Mapigano yalizuka Ijumaa, siku chache baada ya mazungumzo ya amani ya mjini Kampala, Uganda, kuvunjika..


Jeshi DRC linadai kuelekea ngome ya M23


Mwanajeshi wa serikali na ushanga wa risasi, karibu na KIbumba
Ripoti kutoka Jamhuri ya Demokrasi ya Congo zinaeleza kuwa mapigano bado yanaendelea kwa siku ya tatu huku jeshi la serikali likidai kuwa limeuteka mji wa Kibumba, mashariki mwa nchi, na kuwatoa wapiganaji wa kundi la M23.
Kibumba, ilioko kilomita 20 kaskazini ya Goma, ndiko walikokimbilia wapiganaji baada ya kikosi cha Umoja wa Mataifa, MONUSCO, kuwatoa katika mji wa Goma.
Msemaji wa jeshi anaarifiwa kueleza kuwa wameteka miji mengine piya na kwamba jeshi limejigawa na linaelekea kusini upande wa Rutshuru.
Mapigano yalizuka Ijumaa siku chache baada ya mazungumzo ya amani ya mjini Kampala, Uganda, kuvunjika..

No comments:

Post a Comment