Thursday, May 23, 2013

MTUHUMIWA ALIYEMWIBIA MWAJIRI WAKE AFIKISHWA KIZIMBANI TENA MOHAMED ALI MOHAMED

 Mtuhumiwa wa wizi wa shilingi zaidi ya milioni 500 akiingizwa mahakamani.
 Askari wakimsindikiza mtuhumiwa.


Mfanyakazi kampuni ya mafuta ya ABOOS iliyoko mjini BUKOBA, HAMADI ALI MOHAMED anayetuhumiwa kumuibia mwajili wake RAZA FAZAL zaidi ya milioni MIA TANO ISHIRINI na SITA hatimaye amepata dhamana baada ya wadhamini wake kutimiza masharti ya dhamana.
 
 
Mahakama ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Bukoba awali ilitoa masharti ya dhamana kwa kumtaka mtuhumiwa awe na wadhamini WAWILI ambapo mmoja wa wadhamini awe mtumishi wa serikali na mali isiyoamishika yenye thamani zaidi ya shilingi milioni MIA MBILI NA SITINI NA MBILI na mdhamini wa PILI alitakiwa kuwasilisha mahakamani hati ya nyumba yenye thamani ya kiasi hicho.
 
 
Mtuhumiwa huyo mwenye asili ya kiasia aliyepata dhamana baada ya kusota rumande kwa zaidi ya mwezi mmoja alifika kwa mara nyingine kwenye  mahakama ya wilaya ya BUKOBA majira ya saa TATU na NUSU chini ya ulinzi mkali wa askari polisi waliokuwa wamevaa sare za kipolisi  na wengine wakiwa wamevaa nguo za  kiraia.
 
 
Mshitakiwa huyo kufikishwa mahakamani mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya BUKOBA,SYLIVIA LUSHASI, mtuhumiwa hakutakiwa kujibu lolote kufuatia uzito wa kesi inayomkabili, hakimu huyo amesema kesi hiyo itatajwa tena tarehe SITA mwezi JUNI mwaka huu.
 
 
Pamoja na mtuhumiwa huyo kupata dhamana mahakama imemtaka kuwasilisha pasi ya kusafiria pia imemtaka mtuhumiwa huyo kuipa polisi taarifa anapotaka kusafiri toka sehemu moja kwenda nyingine na anatakiwa pia kutosafiri nje ya mkoa wa Kagera.
 
 
 
Mwendesha mashitaka ambaye pia ni wakili wa serikali PAUL KADUSHI akisoma mashitaka yanayomkabili mbele ya hakimu huyo amesema mtuhumiwa anadaiwa kumuibia mwajili zaidi ya shilingi milioni MIA TANO ISHIRINI NA SITA kwa nyakati tofauti kati ya mwezi  JANUARI hadi DESEMBA mwaka 2010.
 

No comments:

Post a Comment