Tuesday, May 21, 2013

MEYA WA MANIPAA YA BUKOBA AENDELEA KUANDAMWA



WAKATI baadhi ya madiwani wa halmashauri ya manispaa wanajiandaa kwenda mjini Dodoma kumuona waziri  mkuu Mizengo Pinda kwa lengo la kumshtaki mstahiki meya wa manispaa hiyo, Anatory Amani  nao baadhi ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi  (CCM) katika manispaa hiyo wameandaa mpango  kurudisha kadi za uanachama wa chama hicho kufuatia  kukerwa na kauli zinazotolewa na meya huyo mara kwa mara.

Wanachama hao wamedai kuwa meya huyo anatakiwa kujiuzulu kwa kuwa miradi yote ya maendeleo ambayo ni pamoja na ujenzi wa soko jipya na upimaji wa viwanja 5,000 kuwa anaibuni kwa maslahi yake binafsi.

Kwa nyakati tofauti wamesema kuwa wamekasirishwa na kauli zake alizozitoa wakati wa kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika siku ya ijumaa iliyopita ya kutumia lugha ya matusi, na pia kuuelea umma kuwa mgogoro kati yak e na wananchi na baadhi ya madiwani wanaompinga umeisha.

Katika kikao hicho Amani aliwambia madiwani kuwa ameishakutana na waziri mkuu hivyo tume iliyoundwa kumchunguza haikubaini tuhuma yoyote inayomkabili.

Meya huyo alichowashangaza wananchi katika kikao hicho alisema ujenzi wa soko jipya la Bukoba utaendelea kama kawaida, walisema kauli aliyoitoa inaingili uhuru wa mahakama kwa kuwa wafanyabiashara ndani ya soko hilo walishafungua kesi ambayo inaendelea kusikilizwa na Mahakama kuu.

No comments:

Post a Comment