Monday, March 25, 2013

JESHI LA POLISI KAGERA LASAMBATARISHA MTANDAO WA MAJAMBAZI

 Silaha mbalimbali zilizonaswa na jeshi la polisi baada ya kuua majambazi matano.
JESHI la polisi mkoani Kagera limefanikiwa kuwaua  watu watano wanatuhumiwa  kujihusisha na vitendo mbalimbali vya uharifu ambavyo ni pamoja wizi wa kutumia silaha na utekaji wa magari kwenye maeneo mbalimbali ya mapori yaliyoko mkoani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa jeshi la polisi wa mkoa wa Kagera, Philip Kalangi amesema jeshi hilo limewaua watu hao  jana baada ya kukutana nao uso kwa uso katika eneo ya msitu wa Kalenge ulioko  wilayani Biharamulo wakati wakitoroka  kuelekea  wilaya ya Kakonko iliyoko mkoani Kigoma.

Anasema watuhumiwa hao baada ya kukutana na askari wa jeshi hilo walianza kurusha risasi ovyo kwa lengo la kujiami, Kalangi amesema pamoja na kurusha risasi hizo  askari hao walifanikiwa kuwazidi nguvu ambapo watuhumiwa wengine walilazimika kukimbilia maporini, watuhumiwa hao walikuwa  na  silaha mbili aina ya SMG,  risasi 35, magazine 2 na simu za mkononi nne, vyote ambavyo viko mikononi mwa jeshi hilo.


Kalangi  amesema waliouwawa walikuwa wakisakwa na jeshi la polisi kwa tuhuma ya kuhusika na tukio la utekaji wa magari manne  uliofanyika  hivi karibuni kwenye maeneo ya Nyamagala yaliyoko Rusaunga wilayani Biharamulo, amesema marehemu walipopekuliwa walikutwa na vitambulisho  vinaonyesha kuwa ni raia wa nchi jirani ya Burundi.

Ametoa wito kwa  wananchi waendelee kushirikiana na jeshi hilo ili liweze kupambana na vitendo vya uharifu ambavyo vinahatarisha amani ndani ya jamii kwa urahisi zaidi,amewaomba wananchi wamtolee taarifa mtu yoyote wanayemtilia mashaka.

No comments:

Post a Comment