Friday, January 04, 2013

HAFLA YA KUWAZAWADIA ASKARI WA JESHI LA POLISI WALIOTEKELEZA WAJIBU WAO VIZURI 2012

 Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe akimpongeza mmoja wa maaskari wa jeshi la polisi waliotekeleza wajibu wao vizuri, askari hao kila mmoja alizawadiwa shilingi 50,000 na cheti maalumu, hafla hiyo ilifanyika kwenye viwanja vya kikosi cha kutuliza ghasia kilichoko eneo la Nshambya lililoko katika manispaa ya Bukoba.
 Askari wa kike nao walizawadiwa.
 Baadhi ya maofisa wa jeshi la polisi waliopata zawadi, kulia ni Shadrack Agumisa na kushoto ni Bw. Rweyongeza maarufu kwa jina la Mamba.
 Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera akiongea wakati wa hafla ya kuwatunuku vyeti na zawadi askari waliotekeleza wajibu wao vizuri.



MKUU wa mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabian Massawe ameushauri uongozi wa jeshi la polisi mkoani humo kuwawajibisha askari wanaokwenda  kinyume na maadili ya kazi yao  ili uweze kulinda heshima ya jeshi hilo.

Massawe alitoa ushauri huo wakati wa hafla fupi ya kuwazawadia maofisa 42 wa jeshi hilo waliotekekeleza wajibu wajibu wao vizuri kwa mwaka 2012 iliandaliwa na jeshi hilo jana na kufanyika kwenye viwanja vya kikosi cha kutuliza ghasia vilivyoko eneo la Nshambya katika manispaa ya Bukoba.

Alisema jeshi la polisi litakapowakumbatia askari wanafachafua sifa ya jeshi la polisi  litakuwa linakaribisha uhasama kati ya jeshi hilo na wananchi ambao mara nyingi ndio huwa vyanzo vya taarifa zinazolisaidia jeshi la polisi kukabiliana na vitendo vya uharifu.

Mkuu huyo wa mkoa alisema jeshi la polisi linapochafuliwa na askari wachache wanaofanya kazi kwa maslahi yao binafsi linaonekana halina dhamana ndani ya jamii, “ndugu  zangu askari pamoja na kufanya kazi nzuri nawaomba kitu kimoja, jueni dhamana yenu ili kila mtu awaheshimu msipofanya hivyo mtakuwa mnakaribisha uadui kati yenu na wananchi” alisema.

“Ndugu zangu maaskari tekelezeni wajibu wenu vizuri hata vyeo haviji kwa njia ya matambiko, vyeo vinatolewa kwa mtu anayetekeleza wajibu wake vizuri, matambiko ya kupata cheo sio kuchinja kuku na mbuzi bali ni kufanya kazi kwa bidii” aliendelea kusema.

Massawe alilipongeza jeshi la polisi kwa kazi nzuri liliyoifanya kwa mwaka 2012 ya kuthibiti matukio ya uharifu yaliyokuwa yamekithiri kwenye mapori ya kimisi na Kasindaga ambayo ni pamoja na unyanganyi wa kutumia silaha, utekaji wa magari na ubakaji.

Aliwataka askari wasibweteke na mafanikio walioyapata badala yake waongeze juhudi katika kutekeleze wajibu wao ili waweze kukomesha kabisa matukio ya uharifu mkoani Kagera, “ninawapongeza sana ndugu zangu maaskari mmefanya kazi nzuri sana nafikiri anayepinga hilo naweza nimlinganisha na bundi ambao huwa wanaona usiku tu” alimaliza.

Kwa upande wake kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera Philip Kalangi alimweleza mkuu wa mkoa kuwa waliozawadiwa ni askari 42 waliofanya kazi vizuri kuanzia mwezi januari hadi Desemba mwaka jana.

Kalangi alisema lengo la jeshi la polisi kuwazadia askari ni kuongeza molali ya kazi, alisema jeshi hili limejiwekea utaratibu wa kutoa zawadi kwa askari wanaofanya vizuri kila mwaka, askari hao kila mmoja alizawadiwa pesa taslimu shilingi 50,000 na cheti cha shukrani.

 Baadhi ya askari na waandishi wa habari.

 Mkuu wa mkoa wa Kagera katika picha ya pamoja na askari waliotunukiwa zawadi na maofisa wengine wa jeshi la polisi.
Maofisa wa jeshi la polisi Kagera wakiwa katika picha ya pamoja.

1 comment:

  1. askari muendelee kufanya kazi kwa bidii mzingatie maelekezo ya massawe

    ReplyDelete