Wednesday, January 30, 2013

Dr. DIODURUS KAMALA ATEMBELEA KIWANDA CHA KUTENGENEZA MBOLEA.

 Dr. Diodorus  Kamala (Balozi wa Tanzania Ubelgiji, Daniel RICHIR Chief Executive Officer wa kampuni ya Rosier na Raphael De RIJCKE General Sales Manager wa kampuni ya Rosier.  Kampuni ya Rosier ni kampuni kubwa inayozalisha mbolea hapa Ubelgiji na na sehemu ya mbolea inayozalishwa na kiwanda hicho inauzwa nchini Tanzania.

 Dr Kamala ameushukuru uongozi wa kiwanda hicho kwa kazi nzuri wanayofanya na pia ameuomba uongozi wa kiwanda hicho kuwatuma watalaamu wake nchini Tanzania ili waweze kuyafanyia utafiti  mazao mbalimbali, udongo na hali ya hewa ya maeneo mbalimbali ya Tanzania.

 Kampuni hiyo imekubali kutuma wataalam Tanzania ili kufanya utafiti utakaosaidia kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya biashara na chakula. Balozi huyo alitembelea  kiwanda hicho jana. Kwa sasa kiwanda hicho kinauzia mbolea Wazalishaji wa Tumbaku . Kiwanda hicho kilianza uzalishaji wa mbolea mwaka 1830, Kinazalisha mbolea za aina mbalimbali kwa kuzingatia mahitaji ya mteja.

No comments:

Post a Comment