Thursday, November 29, 2012

KIKAO CHA MWENYEKITI WA CCM NA WAANDISHI WA HABARI

 Katibu wa Chama Cha Mapinduzi wa mkoa wa Kagera Peter Mushi, akitoa maelezo ya kikao cha Mwenyekiti wa CCM Bi. Costancia Buhiye na waandishi wa habari.
 Baadhi ya wajumbe wa kamati ya siasa na waandishi wa habari.
 Baadhi ya viongozi wa CCM.
 CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kagera kimeiagiza halmashauri ya manispaa ya Bukoba kutoa taarifa sahihi kwa wananchi juu ya miradi inayotekelezwa na itakayotekelezwa ndani ya manispaa hiyo.

Agizo hilo lilitolewa na mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Kagera Bi Costancia Buhiye kwenye taarifa yake aliyoisoma mbele ya wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa wa Kagera na waandishi wa habari alipokutana nao jana kwenye ukumbi wa chama hicho ulioko katika manispaa ya Bukoba.

Katika taarifa hiyo Bi. Buhiye alisema kuwa Halmashauri ya manispaa ya Bukoba ihakikishe inatoa taarifa sahihi  kwa wananchi juu ya miradi ya upimaji wa viwanja na ugawaji 5,000, mradi wa ujenzi wa soko kuu la kisasa la Bukoba na kituo cha mabasi cha kisasa ili haki itendeke kwa kila mwananchi husika.

Bi. Bihuye kwenye taarifa yake hiyo alisema chama kimefikia uamzi wa kutoa agizo hilo baada ya kupokea kwa mguso wa aina ya kipekee hali ya siasa na kiuongozi iliyojitokeza katika manispaa ya Bukoba inayoashiria uvunjifu wa amani na mshikamano.

Alisema kuwa katika kuimarisha mshikamano na kuhakikisha hali ya uvunjifu wa amani katika halmashauri ya manispaa haijitokezi kamati ya siasa ya mkoa wa Kagera imeuagiza uongozi wa CCM wa wilaya ya Bukoba mjini kukaa vikao vya kikatiba kujadili hali ya malumbano na baadae kiweze kuwasilisha mapendekezo ya malumbano hayo kwa uongozi CCM mkoa ili yapatiwe ufumbuzi wa kudumu mapema iwezekanavyo.

Pia aliviomba vyombo vya habari viwaelimishe wananchi wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba wavipuuze vipeperushi ma propoganda zenye nia ya kuwagawa.

"Chama cha mapinduzi tunawaomba wananchi kuendelea kuwa wamoja kwani umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu na umoja ni ushindi kwani pasipo na umoja hapana amani na pasipo amani hakuna maendeleo" alimaliza taarifa yake mwenyekiti huyo.

Taarifa ilitolewa na chama hicho inahusiana na mgogoro uliopo kati ya mstahiki meya wa manispaa ya Bukoba Anatory Amani na waziri wa maliasili na utalii Balozi Khamis Kagasheki, Kagasheki kwenye mkutano wake wa hadhara alioufanya kwenye viwanja vya uhuru aliuambia uongozi wa manispaa ya Bukoba kuweka wazi mikataba ya miradi ya maendeleo inayoiibua ili wananchi waielewe na baadae waikubali.

Alisema wananchi wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba wanapinga miradi ya maendeleo inayoibuliwa katika manispaa hiyo kwa kuwa inafanyika kwa uficho mkubwa hivyo wananchi wanashindwa kuielewa na kusema kuwa ndio maana wananchi baadhi ya miradi wanaipinga, aliitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja mradi wa ujenzi wa soko kuu la Kisasa la Bukoba na  mradi wa upimaji wa viwanja 5,000.

Kagasheki katika mkutano huo alisema kuwa ubabe katika suala zima la kutekeleza miradi inayogusa wananchi kuwa hautakiwe, alisema hatua ya meya Amani kuwatangazia wananchi kupitia kituo kimoja cha radio kuwa iwe isiwe soko litafunjwa mwezi januari ni ya kibabe.

Utekelezwji wa miradi ya maendeleo katika manispaa ya Bukoba sasa imeanza kukumbana na vizingiti ambapo wafanyabiashara  walioko ndani ya soko wamefungua shauri mahakama kuu kupinga kuondolewa ndani ya soko hilo bila kuelezswa hatima yao, pia baadhi ya watu wamefungua kesi mahakamani kupinga mradi wa upimaji wa viwanja wanadai kuwa walikupunjwa wakati wa kulipwa fidia.

 Mkuu wa mkoa wa Kagera alikuwa miongoni mwa walioudhuria kikao hicho.

No comments:

Post a Comment