Wednesday, November 28, 2012

KIKAO CHA KUPASHANA HABARI JUU YA CHANJO ITAKAYOZINDULIWA JANUARI JUU YA MAGONJWA YA NYUMONIA NA KUHARA

 Baadhi ya washiriki wa kikao.

MKUU wa mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu, Fabian Massawe amewaagiza viongozi wa halmashauri za wilaya na manispaa mkoani humo kutunga sheria ndogo ndogo zitakazowabana wazazi wanakataa kuwapeleka watoto wao kwenye vituo  vya afya na zahatati kwa ajili ya kupata chanzo.

Massawe ametoa kauli hiyo wakati wa kikao cha afya ya msingi mkoani Kagera kilichokuwa kinalenga kueleza mikakati ya chanzo mpya ya kuthibiti ugonjwa wa kuhara na rumonia itakayoanza kutolewa mkoani Kagera hivi karibuni kwa watoto chini ya umri wa mwaka mmoja.

Katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkuu huyo wa mkoa leo, Massawe amesema wanakataa kuwapeleka watoto kwenye vituo vya afya na zahanati wanakuwa wanalenga kuchangia ongezeko la vifo hapa nchini kwa watoto hasa walio na umri wa miaka 5.

Amesema kuwa sheria ndogo ndogo  zikitungwa  zitawabana wale wanaoenda kinyume na mikakati ya serikali ya kuhakikisha wananchi wake wanakuwa na afya nzuri, Masaawe amesema kuwa wananchi wanapokuwa na afya nzuri wanachangia sana ukuaji wa kipato cha mtu mmoja mmoja na pato la taifa kwa  ujumla.

Mkuu huyo wa mkoa amesema taifa linaloundwa na watu wenye afya mbovu linadumaa katika Nyanja zote za maendeleo ya kijamii na kiuchumi, aliendelea kusema kuwa kusema kuwa mwitikio wa wazazi kuwapeleka watoto wao kwa ajili ya chanjo unaridhisha.

Akitoa takwimu hali ya halisi ya kiwango cha chanjo mkoani Kagera amesema kuwa kwa mwaka 2009 kiwango cha chanjo mkoani Kagera kilikuwa asilimia 84, 2010 asilimia 87 na  mwaka 2011 kiwango cha chanjo mkoani Kagera kilikuwa asilimia 88.

Kwa upande wake mratibu wa chanjo wa mkoa wa Kagera, Jackson Minja katika kikao hicho amesema kuwa chanzo kwa ajili ya magonjwa ya kuhara na rumonia itatolewa kwa watoto chini ya umri wa mwaka mmoja na chanjo hiyo itaanza kutolewa kuanzia mwaka kesho, mwezi januari.

 Wajumbe wa kikao wakisikiliza Mkuu wa mkoa wa Kagera Bw. Massawe.
 Washiriki wengine wa kikao cha chanjo.
Baadhi ya waratibu wa masuala ya chanjo mkoani Kagera.

No comments:

Post a Comment