Thursday, September 27, 2012

UZINDUZI WA TIGO MAMA AFRIKA SARAKASI WAFANA JIJINI DAR...!!!


Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Leonard Thadeo akizungumza machache katika ufunguzi wa maonyesho ya Tigo Mama AfriKa sarakasi yanayoendelea katika ukumbi wa ukumbi wa Mancom ndani ya Centre New World Cinema Mwenge. Maonyesho hayo yanaendelea mpaka ifikapo Oktoba 4, 2012.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Tigo Tanzania Diego Gutierrez akieleza machache kwa wageni waliokuwa wamefika katika maonyesho hayo.

Mkurugenzi wa Mancom Centre, Constantine Magavilla akiwakaribisha na kuwashukuru wageni waliokuwa wamefika katika uzinduzi wa Tigo Mama Afrika Sarakari.

Moja ya michezo iliyovutia katika Tigo Mama Africa Circus inayoendelea katika ukumbi wa Mancom ndani ya Centre New World Cinema Mwenge.

Huyu kijana anauwezo wa kuendesha baiskeli ya tairi moja.

... ilikuwa ni maajabu na kweli.

Kijana mwingine alionyesha umahili wake ni huyu kama vile unavyomuona.

Michezo ya kamba nayo ilikuwa ya kuvutia.

Mchezo mwingine ulikuwa niwa kurushiana vikapu ya kutimia miguu.

Vijana wakionyesha uhodari wao wa kupaa juu.

Vijana wakiaga mara baada ya onyesho kumalizika.

Wanamuziki wa Bendi ya Inafrika nao wakiaga, kazi yao kubwa ilikuwa ni kusherehesha wakati vijana wakiendelea na onyesho.

Umati mkubwa wa watu uliojitokeza katika maonyesho hayo.

watu walipata fulsa ya kubadilisha mawili matatu. Picha zote na Cathbert Angelo Kajuna wa www.kajunason.blogspot.com

No comments:

Post a Comment